95 : 1
وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيْتُونِ
Naapa kwa tini na zaituni! [1]
95 : 2
وَطُورِ سِينِينَ
Na kwa Mlima wa Sinai! [2]
95 : 3
وَهَـٰذَا ٱلْبَلَدِ ٱلْأَمِينِ
Na kwa mji huu wenye amani! [3]
95 : 4
لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَـٰنَ فِىٓ أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa. [4]
95 : 5
ثُمَّ رَدَدْنَـٰهُ أَسْفَلَ سَـٰفِلِينَ
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini! [5]
95 : 6
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ فَلَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha. [6]
95 : 7
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعْدُ بِٱلدِّينِ
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo? [7]
95 : 8
أَلَيْسَ ٱللَّهُ بِأَحْكَمِ ٱلْحَـٰكِمِينَ
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote? [8]