93 : 1
وَٱلضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana! [1]
★
93 : 2
وَٱلَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda! [2]
★
93 : 3
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe. [3]
★
93 : 4
وَلَلْـَٔاخِرَةُ خَيْرٌ لَّكَ مِنَ ٱلْأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia. [4]
★
93 : 5
وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike. [5]
★
93 : 6
أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi? [6]
★
93 : 7
وَوَجَدَكَ ضَآلًّا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa? [7]
★
93 : 8
وَوَجَدَكَ عَآئِلًا فَأَغْنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza? [8]
★
93 : 9
فَأَمَّا ٱلْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ
Basi yatima usimwonee! [9]
★
93 : 10
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنْهَرْ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie! [10]
★
93 : 11
وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie. [11]
★