92 : 1
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ
Naapa kwa usiku unapo funika! [1]
92 : 2
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na mchana unapo dhihiri! [2]
92 : 3
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ
Na kwa Aliye umba dume na jike! [3]
92 : 4
إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali. [4]
92 : 5
فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa na akamchamngu! [5]
92 : 6
وَصَدَّقَ بِٱلْحُسْنَىٰ
Na akaliwafiki lilio jema! [6]
92 : 7
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْيُسْرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mepesi. [7]
92 : 8
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسْتَغْنَىٰ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake! [8]
92 : 9
وَكَذَّبَ بِٱلْحُسْنَىٰ
Na akakanusha lilio jema! [9]
92 : 10
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْعُسْرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mazito! [10]
92 : 11
وَمَا يُغْنِى عَنْهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia? [11]
92 : 12
إِنَّ عَلَيْنَا لَلْهُدَىٰ
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu. [12]
92 : 13
وَإِنَّ لَنَا لَلْـَٔاخِرَةَ وَٱلْأُولَىٰ
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia. [13]
92 : 14
فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًا تَلَظَّىٰ
Basi nakuonyeni na Moto unao waka! [14]
92 : 15
لَا يَصْلَىٰهَآ إِلَّا ٱلْأَشْقَى
Hatauingia ila mwovu kabisa! [15]
92 : 16
ٱلَّذِى كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Anaye kadhibisha na kupa mgongo. [16]
92 : 17
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلْأَتْقَى
Na mchamngu ataepushwa nao, [17]
92 : 18
ٱلَّذِى يُؤْتِى مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa. [18]
92 : 19
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰٓ
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa. [19]
92 : 20
إِلَّا ٱبْتِغَآءَ وَجْهِ رَبِّهِ ٱلْأَعْلَىٰ
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa. [20]
92 : 21
وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ
Naye atakuja ridhika! [21]