91 : 1
وَٱلشَّمْسِ وَضُحَىٰهَا
Naapa kwa jua na mwangaza wake! [1]
91 : 2
وَٱلْقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapo lifuatia! [2]
91 : 3
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapo lidhihirisha! [3]
91 : 4
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰهَا
Na kwa usiku unapo lifunika! [4]
91 : 5
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga! [5]
91 : 6
وَٱلْأَرْضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza! [6]
91 : 7
وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza! [7]
91 : 8
فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَىٰهَا
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake! [8]
91 : 9
قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Hakika amefanikiwa aliye itakasa! [9]
91 : 10
وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na hakika amekhasiri aliye iviza. [10]
91 : 11
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَىٰهَآ
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao, [11]
91 : 12
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشْقَىٰهَا
Alipo simama mwovu wao mkubwa, [12]
91 : 13
فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقْيَـٰهَا
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake. [13]
91 : 14
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمْ فَسَوَّىٰهَا
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa. [14]
91 : 15
وَلَا يَخَافُ عُقْبَـٰهَا
Wala Yeye haogopi matokeo yake. [15]