89 : 1
وَٱلْفَجْرِ
Naapa kwa alfajiri! [1]
89 : 2
وَلَيَالٍ عَشْرٍ
Na kwa masiku kumi! [2]
89 : 3
وَٱلشَّفْعِ وَٱلْوَتْرِ
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja! [3]
89 : 4
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَسْرِ
Na kwa usiku unapo pita! [4]
89 : 5
هَلْ فِى ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِى حِجْرٍ
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili? [5]
89 : 6
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di? [6]
89 : 7
إِرَمَ ذَاتِ ٱلْعِمَادِ
Wa Iram, wenye majumba marefu? [7]
89 : 8
ٱلَّتِى لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِى ٱلْبِلَـٰدِ
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi? [8]
89 : 9
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُوا۟ ٱلصَّخْرَ بِٱلْوَادِ
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni? [9]
89 : 10
وَفِرْعَوْنَ ذِى ٱلْأَوْتَادِ
Na Firauni mwenye vigingi? [10]
89 : 11
ٱلَّذِينَ طَغَوْا۟ فِى ٱلْبِلَـٰدِ
Ambao walifanya jeuri katika nchi? [11]
89 : 12
فَأَكْثَرُوا۟ فِيهَا ٱلْفَسَادَ
Wakakithirisha humo ufisadi? [12]
89 : 13
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu. [13]
89 : 14
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلْمِرْصَادِ
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia. [14]
89 : 15
فَأَمَّا ٱلْإِنسَـٰنُ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكْرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَكْرَمَنِ
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu! [15]
89 : 16
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَهَـٰنَنِ
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge! [16]
89 : 17
كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ ٱلْيَتِيمَ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima, [17]
89 : 18
وَلَا تَحَـٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ
Wala hamhimizani kulisha masikini; [18]
89 : 19
وَتَأْكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa, [19]
89 : 20
وَتُحِبُّونَ ٱلْمَالَ حُبًّا جَمًّا
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi. [20]
89 : 21
كَلَّآ إِذَا دُكَّتِ ٱلْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande, [21]
89 : 22
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu, [22]
89 : 23
وَجِا۟ىٓءَ يَوْمَئِذٍۭ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَـٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكْرَىٰ
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini? [23]
89 : 24
يَقُولُ يَـٰلَيْتَنِى قَدَّمْتُ لِحَيَاتِى
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu! [24]
89 : 25
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٌ
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake. [25]
89 : 26
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٌ
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake. [26]
89 : 27
يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفْسُ ٱلْمُطْمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyo tua! [27]
89 : 28
ٱرْجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha. [28]
89 : 29
فَٱدْخُلِى فِى عِبَـٰدِى
Basi ingia miongoni mwa waja wangu, [29]
89 : 30
وَٱدْخُلِى جَنَّتِى
Na ingia katika Pepo yangu. [30]