86 : 1
وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku! [1]
86 : 2
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku? [2]
86 : 3
ٱلنَّجْمُ ٱلثَّاقِبُ
Ni Nyota yenye mwanga mkali. [3]
86 : 4
إِن كُلُّ نَفْسٍ لَّمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌ
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi. [4]
86 : 5
فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَـٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani? [5]
86 : 6
خُلِقَ مِن مَّآءٍ دَافِقٍ
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa! [6]
86 : 7
يَخْرُجُ مِنۢ بَيْنِ ٱلصُّلْبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu. [7]
86 : 8
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجْعِهِۦ لَقَادِرٌ
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha. [8]
86 : 9
يَوْمَ تُبْلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Siku zitakapo dhihirishwa siri. [9]
86 : 10
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٍ وَلَا نَاصِرٍ
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi. [10]
86 : 11
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجْعِ
Naapa kwa mbingu yenye marejeo! [11]
86 : 12
وَٱلْأَرْضِ ذَاتِ ٱلصَّدْعِ
Na kwa ardhi inayo pasuka! [12]
86 : 13
إِنَّهُۥ لَقَوْلٌ فَصْلٌ
Hakika hii ni kauli ya kupambanua. [13]
86 : 14
وَمَا هُوَ بِٱلْهَزْلِ
Wala si mzaha. [14]
86 : 15
إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًا
Hakika wao wanapanga mpango. [15]
86 : 16
وَأَكِيدُ كَيْدًا
Na Mimi napanga mpango. [16]
86 : 17
فَمَهِّلِ ٱلْكَـٰفِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًۢا
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole. [17]