84 : 1
إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتْ
Itapo chanika mbingu! [1]
84 : 2
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza! [2]
84 : 3
وَإِذَا ٱلْأَرْضُ مُدَّتْ
Na ardhi itakapo tanuliwa! [3]
84 : 4
وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu! [4]
84 : 5
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza! [5]
84 : 6
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَـٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًا فَمُلَـٰقِيهِ
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta. [6]
84 : 7
فَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَـٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia! [7]
84 : 8
فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi! [8]
84 : 9
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ مَسْرُورًا
Na arudi kwa ahali zake na furaha. [9]
84 : 10
وَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَـٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهْرِهِۦ
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake, [10]
84 : 11
فَسَوْفَ يَدْعُوا۟ ثُبُورًا
Basi huyo ataomba kuteketea. [11]
84 : 12
وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا
Na ataingia Motoni. [12]
84 : 13
إِنَّهُۥ كَانَ فِىٓ أَهْلِهِۦ مَسْرُورًا
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake. [13]
84 : 14
إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena. [14]
84 : 15
بَلَىٰٓ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرًا
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona! [15]
84 : 16
فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلشَّفَقِ
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa, [16]
84 : 17
وَٱلَّيْلِ وَمَا وَسَقَ
Na kwa usiku na unavyo vikusanya, [17]
84 : 18
وَٱلْقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ
Na kwa mwezi unapo pevuka, [18]
84 : 19
لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٍ
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka! [19]
84 : 20
فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
Basi wana nini hawaamini? [20]
84 : 21
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ ٱلْقُرْءَانُ لَا يَسْجُدُونَ ۩
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu? [21]
84 : 22
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ يُكَذِّبُونَ
Bali walio kufuru wanakanusha tu. [22]
84 : 23
وَٱللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria. [23]
84 : 24
فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Basi wabashirie adhabu chungu! [24]
84 : 25
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍۭ
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika. [25]