83 : 1
وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ
Ole wao hao wapunjao! [1]
83 : 2
ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكْتَالُوا۟ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسْتَوْفُونَ
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe. [2]
83 : 3
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza. [3]
83 : 4
أَلَا يَظُنُّ أُو۟لَـٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa . [4]
83 : 5
لِيَوْمٍ عَظِيمٍ
Katika Siku iliyo kuu! [5]
83 : 6
يَوْمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote? [6]
83 : 7
كَلَّآ إِنَّ كِتَـٰبَ ٱلْفُجَّارِ لَفِى سِجِّينٍ
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin. [7]
83 : 8
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سِجِّينٌ
Unajua nini Sijjin? [8]
83 : 9
كِتَـٰبٌ مَّرْقُومٌ
Kitabu kilicho andikwa. [9]
83 : 10
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha! [10]
83 : 11
ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo. [11]
83 : 12
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi. [12]
83 : 13
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَـٰتُنَا قَالَ أَسَـٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale! [13]
83 : 14
كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma. [14]
83 : 15
كَلَّآ إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi. [15]
83 : 16
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُوا۟ ٱلْجَحِيمِ
Kisha wataingia Motoni! [16]
83 : 17
ثُمَّ يُقَالُ هَـٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha. [17]
83 : 18
كَلَّآ إِنَّ كِتَـٰبَ ٱلْأَبْرَارِ لَفِى عِلِّيِّينَ
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin. [18]
83 : 19
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin? [19]
83 : 20
كِتَـٰبٌ مَّرْقُومٌ
Kitabu kilicho andikwa. [20]
83 : 21
يَشْهَدُهُ ٱلْمُقَرَّبُونَ
Wanakishuhudia walio karibishwa. [21]
83 : 22
إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍ
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema. [22]
83 : 23
عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia. [23]
83 : 24
تَعْرِفُ فِى وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ ٱلنَّعِيمِ
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema, [24]
83 : 25
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri, [25]
83 : 26
خِتَـٰمُهُۥ مِسْكٌ ۚ وَفِى ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ ٱلْمُتَنَـٰفِسُونَ
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana. [26]
83 : 27
وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسْنِيمٍ
Na mchanganyiko wake ni Tasniim, [27]
83 : 28
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا ٱلْمُقَرَّبُونَ
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa. [28]
83 : 29
إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجْرَمُوا۟ كَانُوا۟ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ يَضْحَكُونَ
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini. [29]
83 : 30
وَإِذَا مَرُّوا۟ بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana. [30]
83 : 31
وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓا۟ إِلَىٰٓ أَهْلِهِمُ ٱنقَلَبُوا۟ فَكِهِينَ
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi. [31]
83 : 32
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوٓا۟ إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea. [32]
83 : 33
وَمَآ أُرْسِلُوا۟ عَلَيْهِمْ حَـٰفِظِينَ
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao. [33]
83 : 34
فَٱلْيَوْمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ مِنَ ٱلْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri, [34]
83 : 35
عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia. [35]
83 : 36
هَلْ ثُوِّبَ ٱلْكُفَّارُ مَا كَانُوا۟ يَفْعَلُونَ
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda? [36]