82 : 1
إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتْ
Mbingu itapo chanika! [1]
82 : 2
وَإِذَا ٱلْكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتْ
Na nyota zitapo tawanyika! [2]
82 : 3
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ فُجِّرَتْ
Na bahari zitakapo pasuliwa! [3]
82 : 4
وَإِذَا ٱلْقُبُورُ بُعْثِرَتْ
Na makaburi yatapo fukuliwa! [4]
82 : 5
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma. [5]
82 : 6
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَـٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلْكَرِيمِ
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu? [6]
82 : 7
ٱلَّذِى خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha! [7]
82 : 8
فِىٓ أَىِّ صُورَةٍ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga. [8]
82 : 9
كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo. [9]
82 : 10
وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَـٰفِظِينَ
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu, [10]
82 : 11
كِرَامًا كَـٰتِبِينَ
Waandishi wenye hishima, [11]
82 : 12
يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ
Wanayajua mnayo yatenda. [12]
82 : 13
إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍ
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema, [13]
82 : 14
وَإِنَّ ٱلْفُجَّارَ لَفِى جَحِيمٍ
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni; [14]
82 : 15
يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ ٱلدِّينِ
Wataingia humo Siku ya Malipo. [15]
82 : 16
وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَآئِبِينَ
Na hawatoacha kuwamo humo. [16]
82 : 17
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani? [17]
82 : 18
ثُمَّ مَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani? [18]
82 : 19
يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌ لِّنَفْسٍ شَيْـًٔا ۖ وَٱلْأَمْرُ يَوْمَئِذٍ لِّلَّهِ
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu. [19]