81 : 1
إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Jua litakapo kunjwa! [1]
81 : 2
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتْ
Na nyota zikazimwa! [2]
81 : 3
وَإِذَا ٱلْجِبَالُ سُيِّرَتْ
Na milima ikaondolewa! [3]
81 : 4
وَإِذَا ٱلْعِشَارُ عُطِّلَتْ
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe, [4]
81 : 5
وَإِذَا ٱلْوُحُوشُ حُشِرَتْ
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa! [5]
81 : 6
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ سُجِّرَتْ
Na bahari zikawaka moto! [6]
81 : 7
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتْ
Na nafsi zikaunganishwa! [7]
81 : 8
وَإِذَا ٱلْمَوْءُۥدَةُ سُئِلَتْ
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa! [8]
81 : 9
بِأَىِّ ذَنۢبٍ قُتِلَتْ
Kwa kosa gani aliuliwa? [9]
81 : 10
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتْ
Na madaftari yatakapo enezwa, [10]
81 : 11
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتْ
Na mbingu itapo tanduliwa, [11]
81 : 12
وَإِذَا ٱلْجَحِيمُ سُعِّرَتْ
Na Jahannamu itapo chochewa, [12]
81 : 13
وَإِذَا ٱلْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ
Na Pepo ikasogezwa, [13]
81 : 14
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّآ أَحْضَرَتْ
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha. [14]
81 : 15
فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلْخُنَّسِ
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma, [15]
81 : 16
ٱلْجَوَارِ ٱلْكُنَّسِ
Zinazo kwenda, kisha zikajificha, [16]
81 : 17
وَٱلَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ
Na kwa usiku unapo pungua, [17]
81 : 18
وَٱلصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka, [18]
81 : 19
إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu, [19]
81 : 20
ذِى قُوَّةٍ عِندَ ذِى ٱلْعَرْشِ مَكِينٍ
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi, [20]
81 : 21
مُّطَاعٍ ثَمَّ أَمِينٍ
Anaye t'iiwa, tena muaminifu. [21]
81 : 22
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍ
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu. [22]
81 : 23
وَلَقَدْ رَءَاهُ بِٱلْأُفُقِ ٱلْمُبِينِ
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi. [23]
81 : 24
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلْغَيْبِ بِضَنِينٍ
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu. [24]
81 : 25
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَـٰنٍ رَّجِيمٍ
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni. [25]
81 : 26
فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ
Basi mnakwenda wapi? [26]
81 : 27
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَـٰلَمِينَ
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote. [27]
81 : 28
لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa. [28]
81 : 29
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote. [29]