79 : 1
وَٱلنَّـٰزِعَـٰتِ غَرْقًا
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu! [1]
★
79 : 2
وَٱلنَّـٰشِطَـٰتِ نَشْطًا
Na kwa wanao toa kwa upole! [2]
★
79 : 3
وَٱلسَّـٰبِحَـٰتِ سَبْحًا
Na wanao ogelea! [3]
★
79 : 4
فَٱلسَّـٰبِقَـٰتِ سَبْقًا
Wakishindana mbio! [4]
★
79 : 5
فَٱلْمُدَبِّرَٰتِ أَمْرًا
Wakidabiri mambo. [5]
★
79 : 6
يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka! [6]
★
79 : 7
تَتْبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
Kifuate cha kufuatia. [7]
★
79 : 8
قُلُوبٌ يَوْمَئِذٍ وَاجِفَةٌ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga! [8]
★
79 : 9
أَبْصَـٰرُهَا خَـٰشِعَةٌ
Macho yatainama chini! [9]
★
79 : 10
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِى ٱلْحَافِرَةِ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza? [10]
★
79 : 11
أَءِذَا كُنَّا عِظَـٰمًا نَّخِرَةً
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa? [11]
★
79 : 12
قَالُوا۟ تِلْكَ إِذًا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara! [12]
★
79 : 13
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌ وَٰحِدَةٌ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu, [13]
★
79 : 14
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano! [14]
★
79 : 15
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa? [15]
★
79 : 16
إِذْ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia: [16]
★
79 : 17
ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri [17]
★
79 : 18
فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa? [18]
★
79 : 19
وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha. [19]
★
79 : 20
فَأَرَىٰهُ ٱلْـَٔايَةَ ٱلْكُبْرَىٰ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa. [20]
★
79 : 21
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Lakini aliikadhibisha na akaasi. [21]
★
79 : 22
ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi. [22]
★
79 : 23
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Akakusanya watu akanadi. [23]
★
79 : 24
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلْأَعْلَىٰ
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa. [24]
★
79 : 25
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلْـَٔاخِرَةِ وَٱلْأُولَىٰٓ
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo. [25]
★
79 : 26
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَعِبْرَةً لِّمَن يَخْشَىٰٓ
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa. [26]
★
79 : 27
ءَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُ ۚ بَنَىٰهَا
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga! [27]
★
79 : 28
رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri. [28]
★
79 : 29
وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَىٰهَا
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake [29]
★
79 : 30
وَٱلْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi. [30]
★
79 : 31
أَخْرَجَ مِنْهَا مَآءَهَا وَمَرْعَىٰهَا
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake, [31]
★
79 : 32
وَٱلْجِبَالَ أَرْسَىٰهَا
Na milima akaisimamisha, [32]
★
79 : 33
مَتَـٰعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَـٰمِكُمْ
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu. [33]
★
79 : 34
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلْكُبْرَىٰ
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa, [34]
★
79 : 35
يَوْمَ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَـٰنُ مَا سَعَىٰ
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya, [35]
★
79 : 36
وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona, [36]
★
79 : 37
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Basi ama yule aliye zidi ujeuri, [37]
★
79 : 38
وَءَاثَرَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا
Na akakhiari maisha ya dunia, [38]
★
79 : 39
فَإِنَّ ٱلْجَحِيمَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake! [39]
★
79 : 40
وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفْسَ عَنِ ٱلْهَوَىٰ
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio, [40]
★
79 : 41
فَإِنَّ ٱلْجَنَّةَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake! [41]
★
79 : 42
يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini? [42]
★
79 : 43
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ
Una nini wewe hata uitaje? [43]
★
79 : 44
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake. [44]
★
79 : 45
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَىٰهَا
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu. [45]
★
79 : 46
كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوٓا۟ إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَىٰهَا
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake. [46]
★