56 : 1
إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ
Litakapo tukia hilo Tukio . [1]
★
56 : 2
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Hapana cha kukanusha kutukia kwake. [2]
★
56 : 3
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ
Literemshalo linyanyualo! [3]
★
56 : 4
إِذَا رُجَّتِ ٱلْأَرْضُ رَجًّا
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso! [4]
★
56 : 5
وَبُسَّتِ ٱلْجِبَالُ بَسًّا
Na milima itapo sagwasagwa! [5]
★
56 : 6
فَكَانَتْ هَبَآءً مُّنۢبَثًّا
Iwe mavumbi yanayo peperushwa! [6]
★
56 : 7
وَكُنتُمْ أَزْوَٰجًا ثَلَـٰثَةً
Na nyinyi mtakuwa namna tatu: . [7]
★
56 : 8
فَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani? [8]
★
56 : 9
وَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni? [9]
★
56 : 10
وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ
Na wa mbele watakuwa mbele. [10]
★
56 : 11
أُو۟لَـٰٓئِكَ ٱلْمُقَرَّبُونَ
Hao ndio watakao karibishwa [11]
★
56 : 12
فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Katika Bustani zenye neema. [12]
★
56 : 13
ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Fungu kubwa katika wa mwanzo, [13]
★
56 : 14
وَقَلِيلٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ
Na wachache katika wa mwisho. [14]
★
56 : 15
عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa. [15]
★
56 : 16
مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيْهَا مُتَقَـٰبِلِينَ
Wakiviegemea wakielekeana. [16]
★
56 : 17
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌ مُّخَلَّدُونَ
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele, [17]
★
56 : 18
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi. [18]
★
56 : 19
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa. [19]
★
56 : 20
وَفَـٰكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Na matunda wayapendayo, [20]
★
56 : 21
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani. [21]
★
56 : 22
وَحُورٌ عِينٌ
Na Mahurulaini, [22]
★
56 : 23
كَأَمْثَـٰلِ ٱللُّؤْلُؤِ ٱلْمَكْنُونِ
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa. [23]
★
56 : 24
جَزَآءًۢ بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda. [24]
★
56 : 25
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi, [25]
★
56 : 26
إِلَّا قِيلًا سَلَـٰمًا سَلَـٰمًا
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama. [26]
★
56 : 27
وَأَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani? [27]
★
56 : 28
فِى سِدْرٍ مَّخْضُودٍ
Katika mikunazi isiyo na miba, [28]
★
56 : 29
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ
Na migomba iliyo pangiliwa, [29]
★
56 : 30
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ
Na kivuli kilicho tanda, [30]
★
56 : 31
وَمَآءٍ مَّسْكُوبٍ
Na maji yanayo miminika, [31]
★
56 : 32
وَفَـٰكِهَةٍ كَثِيرَةٍ
Na matunda mengi, [32]
★
56 : 33
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ
Hayatindikii wala hayakatazwi, [33]
★
56 : 34
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa. [34]
★
56 : 35
إِنَّآ أَنشَأْنَـٰهُنَّ إِنشَآءً
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya, [35]
★
56 : 36
فَجَعَلْنَـٰهُنَّ أَبْكَارًا
Na tutawafanya vijana, [36]
★
56 : 37
عُرُبًا أَتْرَابًا
Wanapendana na waume zao, hirimu moja. [37]
★
56 : 38
لِّأَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
Kwa ajili ya watu wa kuliani. [38]
★
56 : 39
ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Fungu kubwa katika wa mwanzo, [39]
★
56 : 40
وَثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ
Na fungu kubwa katika wa mwisho. [40]
★
56 : 41
وَأَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni? [41]
★
56 : 42
فِى سَمُومٍ وَحَمِيمٍ
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka, [42]
★
56 : 43
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ
Na kivuli cha moshi mweusi, [43]
★
56 : 44
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ
Si cha kuburudisha wala kustarehesha. [44]
★
56 : 45
إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa. [45]
★
56 : 46
وَكَانُوا۟ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلْحِنثِ ٱلْعَظِيمِ
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa, [46]
★
56 : 47
وَكَانُوا۟ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa? [47]
★
56 : 48
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
Au baba zetu wa zamani? [48]
★
56 : 49
قُلْ إِنَّ ٱلْأَوَّلِينَ وَٱلْـَٔاخِرِينَ
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho [49]
★
56 : 50
لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu. [50]
★
56 : 51
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلْمُكَذِّبُونَ
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha, [51]
★
56 : 52
لَـَٔاكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu. [52]
★
56 : 53
فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
Na kwa mti huo mtajaza matumbo. [53]
★
56 : 54
فَشَـٰرِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ ٱلْحَمِيمِ
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka. [54]
★
56 : 55
فَشَـٰرِبُونَ شُرْبَ ٱلْهِيمِ
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu. [55]
★
56 : 56
هَـٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ ٱلدِّينِ
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo. [56]
★
56 : 57
نَحْنُ خَلَقْنَـٰكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki? [57]
★
56 : 58
أَفَرَءَيْتُم مَّا تُمْنُونَ
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza? [58]
★
56 : 59
ءَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلْخَـٰلِقُونَ
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji? [59]
★
56 : 60
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ ٱلْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi [60]
★
56 : 61
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَـٰلَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِى مَا لَا تَعْلَمُونَ
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua. [61]
★
56 : 62
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ ٱلنَّشْأَةَ ٱلْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki? [62]
★
56 : 63
أَفَرَءَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda? [63]
★
56 : 64
ءَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلزَّٰرِعُونَ
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha? [64]
★
56 : 65
لَوْ نَشَآءُ لَجَعَلْنَـٰهُ حُطَـٰمًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu, [65]
★
56 : 66
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika; [66]
★
56 : 67
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
Bali sisi tumenyimwa. [67]
★
56 : 68
أَفَرَءَيْتُمُ ٱلْمَآءَ ٱلَّذِى تَشْرَبُونَ
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa? [68]
★
56 : 69
ءَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ ٱلْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنزِلُونَ
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha? [69]
★
56 : 70
لَوْ نَشَآءُ جَعَلْنَـٰهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru? [70]
★
56 : 71
أَفَرَءَيْتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِى تُورُونَ
Je! Mnauona moto mnao uwasha? [71]
★
56 : 72
ءَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَآ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنشِـُٔونَ
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji? [72]
★
56 : 73
نَحْنُ جَعَلْنَـٰهَا تَذْكِرَةً وَمَتَـٰعًا لِّلْمُقْوِينَ
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani. [73]
★
56 : 74
فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu. [74]
★
56 : 75
۞ فَلَآ أُقْسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ
Basi naapa kwa maanguko ya nyota, [75]
★
56 : 76
وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua! [76]
★
56 : 77
إِنَّهُۥ لَقُرْءَانٌ كَرِيمٌ
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu, [77]
★
56 : 78
فِى كِتَـٰبٍ مَّكْنُونٍ
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa. [78]
★
56 : 79
لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلْمُطَهَّرُونَ
Hapana akigusaye ila walio takaswa. [79]
★
56 : 80
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. [80]
★
56 : 81
أَفَبِهَـٰذَا ٱلْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza? [81]
★
56 : 82
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha? [82]
★
56 : 83
فَلَوْلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلْحُلْقُومَ
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo, [83]
★
56 : 84
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ
Na nyinyi wakati huo mnatazama! [84]
★
56 : 85
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَـٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi. [85]
★
56 : 86
فَلَوْلَآ إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu, [86]
★
56 : 87
تَرْجِعُونَهَآ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli? [87]
★
56 : 88
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa, [88]
★
56 : 89
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema. [89]
★
56 : 90
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنْ أَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia, [90]
★
56 : 91
فَسَلَـٰمٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia. [91]
★
56 : 92
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu, [92]
★
56 : 93
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka, [93]
★
56 : 94
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ
Na kutiwa Motoni. [94]
★
56 : 95
إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلْيَقِينِ
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini. [95]
★
56 : 96
فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa. [96]
★