55 : 1
ٱلرَّحْمَـٰنُ
Arrah'man, Mwingi wa Rehema .
★
55 : 2
عَلَّمَ ٱلْقُرْءَانَ
Amefundisha Qur'ani. [2]
★
55 : 3
خَلَقَ ٱلْإِنسَـٰنَ
Amemuumba mwanaadamu!
★
55 : 4
عَلَّمَهُ ٱلْبَيَانَ
Akamfundisha kubaini.
★
55 : 5
ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ بِحُسْبَانٍ
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
★
55 : 6
وَٱلنَّجْمُ وَٱلشَّجَرُ يَسْجُدَانِ
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
★
55 : 7
وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلْمِيزَانَ
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani!
★
55 : 8
أَلَّا تَطْغَوْا۟ فِى ٱلْمِيزَانِ
Ili msidhulumu katika mizani.
★
55 : 9
وَأَقِيمُوا۟ ٱلْوَزْنَ بِٱلْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا۟ ٱلْمِيزَانَ
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
★
55 : 10
وَٱلْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
★
55 : 11
فِيهَا فَـٰكِهَةٌ وَٱلنَّخْلُ ذَاتُ ٱلْأَكْمَامِ
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
★
55 : 12
وَٱلْحَبُّ ذُو ٱلْعَصْفِ وَٱلرَّيْحَانُ
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
★
55 : 13
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
★
55 : 14
خَلَقَ ٱلْإِنسَـٰنَ مِن صَلْصَـٰلٍ كَٱلْفَخَّارِ
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo.
★
55 : 15
وَخَلَقَ ٱلْجَآنَّ مِن مَّارِجٍ مِّن نَّارٍ
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
★
55 : 16
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
★
55 : 17
رَبُّ ٱلْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ ٱلْمَغْرِبَيْنِ
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
★
55 : 18
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 19
مَرَجَ ٱلْبَحْرَيْنِ يَلْتَقِيَانِ
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
★
55 : 20
بَيْنَهُمَا بَرْزَخٌ لَّا يَبْغِيَانِ
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
★
55 : 21
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 22
يَخْرُجُ مِنْهُمَا ٱللُّؤْلُؤُ وَٱلْمَرْجَانُ
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
★
55 : 23
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 24
وَلَهُ ٱلْجَوَارِ ٱلْمُنشَـَٔاتُ فِى ٱلْبَحْرِ كَٱلْأَعْلَـٰمِ
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
★
55 : 25
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 26
كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
★
55 : 27
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو ٱلْجَلَـٰلِ وَٱلْإِكْرَامِ
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
★
55 : 28
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 29
يَسْـَٔلُهُۥ مَن فِى ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِى شَأْنٍ
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
★
55 : 30
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 31
سَنَفْرُغُ لَكُمْ أَيُّهَ ٱلثَّقَلَانِ
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
★
55 : 32
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 33
يَـٰمَعْشَرَ ٱلْجِنِّ وَٱلْإِنسِ إِنِ ٱسْتَطَعْتُمْ أَن تَنفُذُوا۟ مِنْ أَقْطَارِ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ فَٱنفُذُوا۟ ۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلْطَـٰنٍ
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
★
55 : 34
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 35
يُرْسَلُ عَلَيْكُمَا شُوَاظٌ مِّن نَّارٍ وَنُحَاسٌ فَلَا تَنتَصِرَانِ
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
★
55 : 36
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 37
فَإِذَا ٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ وَرْدَةً كَٱلدِّهَانِ
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
★
55 : 38
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 39
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُسْـَٔلُ عَن ذَنۢبِهِۦٓ إِنسٌ وَلَا جَآنٌّ
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
★
55 : 40
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 41
يُعْرَفُ ٱلْمُجْرِمُونَ بِسِيمَـٰهُمْ فَيُؤْخَذُ بِٱلنَّوَٰصِى وَٱلْأَقْدَامِ
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
★
55 : 42
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 43
هَـٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِى يُكَذِّبُ بِهَا ٱلْمُجْرِمُونَ
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
★
55 : 44
يَطُوفُونَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ حَمِيمٍ ءَانٍ
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
★
55 : 45
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 46
وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
★
55 : 47
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 48
ذَوَاتَآ أَفْنَانٍ
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
★
55 : 49
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 50
فِيهِمَا عَيْنَانِ تَجْرِيَانِ
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
★
55 : 51
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 52
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَـٰكِهَةٍ زَوْجَانِ
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
★
55 : 53
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 54
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ فُرُشٍۭ بَطَآئِنُهَا مِنْ إِسْتَبْرَقٍ ۚ وَجَنَى ٱلْجَنَّتَيْنِ دَانٍ
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
★
55 : 55
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 56
فِيهِنَّ قَـٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَآنٌّ
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
★
55 : 57
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 58
كَأَنَّهُنَّ ٱلْيَاقُوتُ وَٱلْمَرْجَانُ
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
★
55 : 59
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
★
55 : 60
هَلْ جَزَآءُ ٱلْإِحْسَـٰنِ إِلَّا ٱلْإِحْسَـٰنُ
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
★
55 : 61
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 62
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
★
55 : 63
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 64
مُدْهَآمَّتَانِ
Za kijani kibivu.
★
55 : 65
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 66
فِيهِمَا عَيْنَانِ نَضَّاخَتَانِ
Na chemchem mbili zinazo furika.
★
55 : 67
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 68
فِيهِمَا فَـٰكِهَةٌ وَنَخْلٌ وَرُمَّانٌ
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
★
55 : 69
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 70
فِيهِنَّ خَيْرَٰتٌ حِسَانٌ
Humo wamo wanawake wema wazuri.
★
55 : 71
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 72
حُورٌ مَّقْصُورَٰتٌ فِى ٱلْخِيَامِ
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
★
55 : 73
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 74
لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَآنٌّ
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
★
55 : 75
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 76
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ رَفْرَفٍ خُضْرٍ وَعَبْقَرِىٍّ حِسَانٍ
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
★
55 : 77
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
★
55 : 78
تَبَـٰرَكَ ٱسْمُ رَبِّكَ ذِى ٱلْجَلَـٰلِ وَٱلْإِكْرَامِ
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
★