104 : 1
وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ
Ole wake kila safihi, msengenyaji! [1]
★
104 : 2
ٱلَّذِى جَمَعَ مَالًا وَعَدَّدَهُۥ
Aliye kusanya mali na kuyahisabu. [2]
★
104 : 3
يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخْلَدَهُۥ
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! [3]
★
104 : 4
كَلَّا ۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِى ٱلْحُطَمَةِ
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. [4]
★
104 : 5
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْحُطَمَةُ
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? [5]
★
104 : 6
نَارُ ٱللَّهِ ٱلْمُوقَدَةُ
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. [6]
★
104 : 7
ٱلَّتِى تَطَّلِعُ عَلَى ٱلْأَفْـِٔدَةِ
Ambao unapanda nyoyoni. [7]
★
104 : 8
إِنَّهَا عَلَيْهِم مُّؤْصَدَةٌ
Hakika huo utafungiwa nao [8]
★
104 : 9
فِى عَمَدٍ مُّمَدَّدَةٍۭ
Kwenye nguzo zilio nyooshwa. [9]
★