102 : 1
أَلْهَىٰكُمُ ٱلتَّكَاثُرُ
Kumekushughulisheni kutafuta wingi, [1]
★
102 : 2
حَتَّىٰ زُرْتُمُ ٱلْمَقَابِرَ
Mpaka mje makaburini! [2]
★
102 : 3
كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ
Sivyo hivyo! Mtakuja jua! [3]
★
102 : 4
ثُمَّ كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ
Tena sivyo hivyo! Mtakuja jua! [4]
★
102 : 5
كَلَّا لَوْ تَعْلَمُونَ عِلْمَ ٱلْيَقِينِ
Sivyo hivyo! Lau mngeli jua kwa ujuzi wa yakini, [5]
★
102 : 6
لَتَرَوُنَّ ٱلْجَحِيمَ
Basi bila ya shaka mtaiona Jahannamu! [6]
★
102 : 7
ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيْنَ ٱلْيَقِينِ
Tena, bila ya shaka, mtaiona kwa jicho la yakini. [7]
★
102 : 8
ثُمَّ لَتُسْـَٔلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ
Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema. [8]
★