101 : 1
ٱلْقَارِعَةُ
Inayo gonga! [1]
101 : 2
مَا ٱلْقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga? [2]
101 : 3
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْقَارِعَةُ
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? [3]
101 : 4
يَوْمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلْفَرَاشِ ٱلْمَبْثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; [4]
101 : 5
وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ ٱلْمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! [5]
101 : 6
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, [6]
101 : 7
فَهُوَ فِى عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. [7]
101 : 8
وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَٰزِينُهُۥ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, [8]
101 : 9
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٌ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! [9]
101 : 10
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا هِيَهْ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? [10]
101 : 11
نَارٌ حَامِيَةٌۢ
Ni Moto mkali! [11]