100 : 1
وَٱلْعَـٰدِيَـٰتِ ضَبْحًا
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua, [1]
100 : 2
فَٱلْمُورِيَـٰتِ قَدْحًا
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini, [2]
100 : 3
فَٱلْمُغِيرَٰتِ صُبْحًا
Wakishambulia wakati wa asubuhi, [3]
100 : 4
فَأَثَرْنَ بِهِۦ نَقْعًا
Huku wakitimua vumbi, [4]
100 : 5
فَوَسَطْنَ بِهِۦ جَمْعًا
Na wakijitoma kati ya kundi, [5]
100 : 6
إِنَّ ٱلْإِنسَـٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٌ
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi! [6]
100 : 7
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌ
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo! [7]
100 : 8
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلْخَيْرِ لَشَدِيدٌ
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali! [8]
100 : 9
۞ أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِى ٱلْقُبُورِ
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini? [9]
100 : 10
وَحُصِّلَ مَا فِى ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliomo vifuani? [10]
100 : 11
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّخَبِيرٌۢ
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote! [11]